Monday, 10 August 2015

UTANGULIZI WA RASILIMALI YA MAJI BONDE LA ZIWA NYASA TUKUYU



Maji ni muhimu kiuchumi, kijamii na

kimazingira.
Matumizi ya maji yanapozidi uwezo wa vyanzo husababisha upungufu na kupeleka ukosefu wa maji Kimsingi usimamizi na ugawaji wa maji unahitajika. Tunatambua kuwa Maji yote ni mali ya Taifa na yanasimamiwa chini ya sheria ya usimamizi wa rasilimali za maji Na. 11 ya mwaka 2009.Lengo la sheria hii ni kuratibu na kusimamia matumizi ya maji na kuzuia uchafuzi wa vyanzo. Kila mtu aliyechukua au anayetaka kuchukua maji kwa matumizi yoyote anapaswa kuwa na hati ya kumiliki maji.
 LNBWB ni nini ?

LNBWB ni ofisi inayosimamia na kuratibu 

matumizi ya bonde la Ziwa Nyasa.

Ni yapi majukumu ya Ofisi ya Bonde la Ziwa Nyasa? 

 Kusimamia na kuratibu matumizi bora ya maji. Kudhibiti na 

kuchukua hatua dhidi ya wachafuzi wa 

maji na vyanzo vyake. kutoa vibali vya kutumia maji

Ni changamoto gani zipo katika usimamizi wa

          rasilimali za maji?

 Watu wengi wamekuwa wanatumia maji bila vibali.  Matumizi

makubwa ya maji zaidi ya kiwango kinachohitajika. Watu wengi 

wana imani kuwa maji ni zawadi toka kwa Mungu na 

haipaswi kulipiwa kama rasilimali nyingine. Uharibifu 
mkubwa 

katika vyanzo vya maji kutokana na ongezeko la watu. Upungufu wa maji katika vyanzo vingi

 Bodi ya Maji ya Bonde imechukua hatua gani 

katika kusimamia vyanzo vya maji na kuwa na

uhakika wa maji

    Bodi ya Maji ya Bonde la Ziwa Nyasa katika kulinda na kutunza

vyanzo vya maji,imeweza kuainisha vyanzo vya maji na 
kushirikisha jamii husika katika 



UNAFAIDIKA NA NINI HUDUMA 

ZITOLEWAZO.



                 Huduma zitolewazo........................

  1. Kupata kibali kinachokulinda kisheria 
  2.   Visima vingi hukauka mara kwa mara, kutokana na kutofuata taratibu za uchimbaji na kutokuwa na utafiti wa kina. Sajili kisima chako katika Ofisi za Bonde ili kisima chako kiwe na uhakika wa maji.
  3. Ofisi ya Bonde ndio inayoweza kukupa utatuzi wa migogoro ya matumizi ya Maji.
  4. Kupitia jumuiya za watumia maji,vidakio,na bodi ya bonde znakushirikisha katika  katika suala zima l;a usimamizi wa rasili mali maji

                       BONDE LA ZIWA NYASA
Hili ni eneo lote ambalo mwelekeo wa maji yake hatimaye huingia kaitka Ziwa Nyasa .
Eneo hili linajumuisha mikoa ya Mbeya,Njombe na Ruvuma.

Wateja wengi wamenufaika na huduma zetu 485 Makampuni mashirika na Tasisi za binafsi wanavibali vya maji.

Kwa maelezo zaidi fika Ofisi ya Bonde ya Ziwa Nyasa Tukuyu
 Wizara ya Maji
OfisiyaBonde la ZiwaNyasa
P.O. Box240 TUKUYU
+255 2552250
nyasabasin@yahoo.com
www.lakenyasabasin.com

Ofisi Ndogo Songea
P.O. Box 42, SONGEA
+25525260166
nyasabasinsuboffice@yahoo.com
www.lakenyasabasin.com

No comments:

Post a Comment